Kiswahili Form Six Midterm Exam September 2026 – Mbinga Girls Secondary School
KISWAHILI FORM SIX MIDTERM EXAM SEPTEMBER 2026 – MBINGA
GIRLS SECONDARY SCHOOL
SEHEMU: B (ALAMA 60)
Jibu maswali (03) kutoka sehemu hii. swali la (5) ni la
lazima.
5. Uchanganuzi wa sentensi hufanywa hatua kwa hatua.
Bainisha hatua tano za uchanganuzi wa sentensi kidhima. Kisha changanua
sentensi isemayo “Msichana mnene ananiangalia vibaya”. Tumia njia ya matawi na
kwa mkabala wa kidhima.
6. “Silabi huwa na ruwaza mbalimbali” kwa mifano bayana,
Bainisha ruwaza kuu tano (5) za silabi za Kiswahili.
7. Kwa kutumia mifano ya kiswahili, bainisha miundo mitano
ya kirai nomino (KN).
8. Uainishaji wa sentensi za kiswahili umejikita katika
vigezo vikuu viwili, kwa kutumia mifano maridhawa, bainisha aina za sentesi za
kiswahili kwa kigezo cha kidhima.
